KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, August 29, 2015

TFF YATUMA RAMBIRAMBI KIFO CHA MANDO

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limetuma salam za rambi rambi kwa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa pwani (COREFA) kufuatia kifo cha mwamuzi mstaafu wa FIFA na kamishina wa TFF, Gilbert Mando kilichotokea jana mjini Bagamyoyo.

Kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini, TFF inawapa pole familia ya marehemu, ndugu jamaa na marafiki na kusema wako pamoja katika kipindi hichi kigumu cha maombolezo.

Marehemu Gilbert Mando alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya figo mpaka umauti ulipomfika jana jioni nyumbani kwake eneo la Bong’wa Bagamoyo, taratibu za mazishi zinaendelea nyumbani kwa marehemu.

No comments:

Post a Comment