KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, August 22, 2015

MKWASA ATANGAZA KIKOSI CHA STARS KINACHOKWENDA UTURUKI KESHO



Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro, Charles Mkwasa ametoa orodha ya wachezaji 22 watakaosafiri usiku wa Jumapili kuelekea nchini Uturuki kwa kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria Septemba 05, 2015.

Orodha hiyo ya wachezaji 22 imetoka katika kikosi kilichotangazwa wiki mbili zilizopita na kocha mkuu wa Taifa Stars, ambapo walipata nafasi ya kufanya mazoezi kwa takribani wiki moja katika uwanja wa Karume.

Wachezaji wote waliochaguliwa timu ya Taifa wanapaswa kuripoti kambini Tansoma Hoteli siku ya Jumapili saa 5 asubuhi kwa maandalizi ya mwisho ya safari hiyo.

Wachezaji waliochaguliwa ni All Mustafa (Yanga SC), Aishi Manula (Azam FC), Said Mohamed (Mtibwa Sugar), walinzi Shomari Kapombe (Azam FC), Abdi Banda, Mohamed Hussein, Hassan Isihaka (Simba SC), Juma Abdul, Haji Mngwali, Kelvin Yondani, Nadir Haroub (Yanga SC).

Viungo Mudathir Yahya, Himid Mao, Frank Domayo (Azam FC), Salum Telela, Deus Kaseke (Yanga SC), Said Ndemla (Simba SC), Washambuliaji John Bocco, Farid Musa, (Azam FC), Rashid Mandawa (Mwadui FC), Saimon Msuva (Yanga SC), na Ibrahim Ajib (Simba SC).

Taifa Stars inatarajiwa kuondoka jumapili usiku kwa usafiri wa shirika la ndege la Uturuki (Turkish Airlines), na kufika jumatatu asubuhi jijini Istambul, ambapo timu itaelekea katika mji wa Kocael ambapo itaweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya Green Park Kartepe

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limetuma salam za rambi rambi kwa chama cha mpira wa miguu mkoa wa Pwani (COREFA) kufuatia kifo cha mwamuzi mstaafu wa mpira miguu Rajabu Zarara kilichotokea juzi usiku jijini Dar es salam.

Marehemu Zarara licha ya kuwa mwamuzi alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Waamuzi mkoa wa Pwani, amezikwa jana jijini Dar es salaam.

TFF pia imetuma salam za rambi rambi kwa Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, kufuatia kifo cha mwanachama wake Athuman Makaranga kilichotokea leo asubuhi jijni Dar es salaam.

Makaranga alikuwa ni mwanachama wa klabu hiyo miongoni wa wadau wa mpira wa miguu, ambapo alishiriki vyema kwenye michuano ya Kagame iliyomalizika hivi karibuni.

TFF kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini inawapa pole wafiwa, ndugu, jamaa na marafiki wote kufuatia misiba hiyo na kusema iko pamoja nao katika kipindi hiki cha maombolezo

No comments:

Post a Comment