KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, August 28, 2015

TFF YAMPONGEZA BAYI


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi ametuma salam za pongezi kwa katibu mkuu wa TOC nchini Filbert Bayi kwa kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya Shirikisho la Riadha Duniani (IAAF).

Katika salam zake Malinzi amempongeza Bayi kwa kuchaguliwa katika nafasi hiyo muhimu ya kutunga na kupitisha sheria zinazotumika katika michezo ya Olimpiki Duniani.

Bayi amechaguliwa katika nafasi hiyo ya Mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya Olimpiki dunanI katika uchaguzi uliofanyika nchini China, ambapo ataitumikia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minne.

Kwa niaba ya famili ya mpira wa miguu nchini, TFF inamtakia kila la kheri FIilbert Bayi katika nafasi hiyo aliyochaguliwa na kuahidi kuendelea kushirkiana nae katika kuendeleza michezo nchini

No comments:

Post a Comment