KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, August 28, 2015

MISRI YAJITOA ALL AFRICAN GAMES


Nchi ya Misri imetangaza kujiondoa dakika za mwisho kushiriki kwenye fainali za Michezo ya Afrika (All Africa Games) kwa timu zake za Wanawake na Wanaume, fainali zinazotarajiwa kuanza kutimu vumbi mwezi Septemba nchini Congo- Brazzavile.

Kwa mujibu wa kifungu cha 19 (B) cha uendeshaji wa michuano hiyo kinasema “Kama timu itajiondoa baada ya kuwa imeshafuzu kwa hatua ya fainali, lakini kabla ya kuanza kwa michezo yenyewe, Kamati ya Uendeshaji wa Mashindano itaziba nafasi hiyo kwa kuteua timu iliyotolewa katika hatua ya mwisho”.

Kujitoa kwa timu za wanawake na wanaume za Misri, kunatoa nafasi kwa Kamati ya Uendeshaji wa Mashindano kuzipa nafasi timu za Senegali (Wanawake), na Burundi (Wanaume) ambazo zilitolewa na Misri katika hatua ya mwisho.

Misri ilipangwa katika kundi B kwa Wanawake na timu za Cameroon, Ghana na Afrika Kusini, huku timu ya Wanaume ikiwa kundi B na timu za Ghana, Senegal na Nigeria

Wakati huo huo Mwamuzi Ferdinand Chacha kutoka Tanzania ameteuliwa kuwa miongoni wa waamuzi wa michuano ya Michezo ya Afrika (All Africa Games) nchini Congo-Brazzavile.

TFF inampongeza Chacha na kumtakia kila la kheri katika kuipeperusha bendera ya Tanzania katika michuano hiyo

No comments:

Post a Comment