KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 30, 2017

WAGOMBEA 29 WAFANYIWA USAILI TFF



Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limefanya usaili kwa wagombea 29 wa nafasi mbalimbali katika siku ya kwanza ya hatua hiyo muhimu kuelekea uchaguzi mkuu wa shirikisho.

Kabla ya usaili, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Revocatus Kuuli, aliwatangazia wagombea wote kuwa amepokea mapingamzi mawili ambayo ni:-

Hussein Mwamba ambaye ni Mjumbe kwa sasa wa Kamati ya Utendaji ya TFF, aliyempinga Mussa Sima kuwa amejitokeza kuwania nafasi hiyo katika Kanda ya 10 ya Mikoa ya Dodoma na Singida kuwa hana uzoefu wa miaka mitano.

Wanafamilia wote kwa maana ya Mwamba na Sima walikuwako. Wakaitwa kikaoni, lakini mweka pingamizi – Mwamba aliamua kulitoa pingamizi lake.

Pingamizi jingine ambalo liliwekwa leo ni kwa Mgombea nafasi ya urais John Kijumbe ambaye anapinga Wallace Karia – Makamu Rais kwa sasa wa TFF kwamba hana sifa za kuwania urais wa TFF kama alivyoomba.

Hata hivyo, pingamizi hilo halijasikilizwa kwa sababu ya wahusika wote kutokuwako na baada ya kamati kufanya nao mawasiliano, wametangaza kusikiliza pingamizi hilo Jumamosi ambayo ni siku ya mwisho ya usaili.

Wagombea ambao wamesailiwa leo hadi jioni ya leo Alhamisi kwa upande wa wagombea urais ni Imani Madega na Ally Mayay wakati Wagombea Makamu urais waliosailiwa ni Mtemi Ramadhani na Mulamu Nghambi.

Kanda Na. 1 Mikoa ya Kagera na Geita;

Soloum Chama

Kaliro Samson

Leopold Mukebezi

Kanda Na. 2 Mikoa ya Mara na Mwanza;

Aaron Nyanda

Samwel Daniel

Bado

Vedastus Lufano

Ephraim Majinge

Kanda Na. 3 Mikoa ya Shinyanga na Simiyu;

Mbasha Matutu

Bado

Benista Rugora

Stanslaus Nyongo

Kanda Na. 4 Mikoa ya Arusha na Manyara;

Wote Bado

Omari Walii

Sarah Chao

Peter Temu

Kanda Na. 5 Mikoa ya Kigoma na Tabora;

John Kadutu

Bado

Issa Bukuku

Abubakar Zebo

Francis Michael

Kanda Na. 6 Mikoa ya Katavi na Rukwa;

Baraka Mazengo

Bado

Kenneth Pesambili

Kanda Na. 7 Mikoa ya Mbeya, Songwe na Iringa;

Elias Mwanjala

Cyprian Kuyava

Bado

Erick Ambakisye

Abousuphyan Silliah

Kanda Na. 8 Mikoa ya Njombe na Ruvuma;

Wote bado

James Mhagama

Golden Sanga

Vicent Majili

Yono Kevela

Kanda Na. 9 Lindi na Mtwara;

Wote Bado

Athuman Kambi

Dunstan Mkundi

Kanda Na. 10 Mikoa ya Dodoma na Singida;

Hussein Mwamba

Mohamed Aden

Musa Sima

George Benedict Komba

Bado

Stewart Masima

 Ally Suru

Kanda Na. 11 Mikoa ya Pwani na Morogoro;

Gabriel Mkwawe

Bado

Charles Mwakambaya

Francis Ndulane

Hassan Othman ‘Hassanol’

Kanda ya 12. Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga

Khalid Mohamed

Bado

Goodluck Moshi

Thabit Kandoro

Kanda Na. 13 Mkoa wa Dar es Salaam

Emmanuel Ashery

Shaffih Dauda

Mussa Kisoky

Lameck Nyambaya

Jamhuri Kihwelo

Saad Kawemba

Bado

Bakari Malima

Ayoub Nyenzi

Saleh Alawi

Ramadhani Nassib

 Aziz Khalfan

Abdul Sauko

Peter Mhinzi

Ally Kamtande

Said Tully

No comments:

Post a Comment