KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 30, 2017

MAKOCHA 19 WAFUZU KOZI YA DARAJA A YA CAF


Makocha 19 wa mpira wa miguu, wamehitimu kozi ya Daraja ‘A’ ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) iliyofanyika Makao Makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), iliyoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.

Makocha hao walimaliza gwe ya pili ya siku 19, katika kozi hiyo ambayo mbali ya kuwa na wakufunzi wengine, wakufunzi wakuu wa CAF walikuwa ni Athumani Lubowa na Sunday Kayuni.

Kayuni ambaye ni Mkurugenzi wa zamani wa TFF katika kozi hii amehudumu kama mkufunzi mkuu wa CAF na aliyekuja kuwasimamia (Accessor) ni Mkurugenzi wa sasa wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Uganda, Athumani Lubowa.

Makocha waliohitimu ni Kidao Wilfred Mzigama, Ali Vuai Shein, Wane Nelson Mkisi, Abdulmutik Haji Ali, Hababuu Ali Omar, Meck Maxime Kianga, Salim Ali Haji, Malale Hamsini Keya na Abdallah Mohammed Juma.

Wengine ni Salim Juma Makame, Emmanuel Raymond Massawe, Mohammed Alawdin Tajdin, Fikiri Elias Mahiza, Juma Ramadhani Mgunda na Dismas Gordon Haonga, Abdul Hassan Banyai, Maka Andrew Mwalwisi, Dennis Mrisho Kitambi na Sebastian Leonard Nkoma.

Akifunga kozi hiyo, Mgeni rasmi Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa TFF, Khalid Mohammed Abdallah aliwatakia kila la kheri kwa makocha hao akiwaelezea kuwa wamejaa utajiri wa ufundi ambao hawana budi kuutendea haki kwa kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya mpira wa miguu.

Awali, akizungumzia wahitimu hao, Mkufunzi Lubowa alisema kwamba anamini makocha hao watafanya vema kwa kuwa katika kipindi chote cha kozi, walionyesha kuwa na nidhamu ya hali ya juu – alama kuu ya mafanikio.

No comments:

Post a Comment