KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, June 18, 2017

HATIMAYE MKUDE AMWAGA WINO SIMBA


Hatimaye Nahodha wa klabu ya Simba, Jonas Mkude amezima ndoto za Yanga baada ya kuongeza mkataba na klabu yake hiyo wa miaka miwili wa kukitumikia kikosi cha mabingwa wa Kombe la FA.

Kulikuwa na mvutano na timu yake kwa dau kubwa ambalo alilokuwa anataka huku kukienea tetezi kuwa mahasimu wao wakubwa Yanga walikuwa wanamhitaji hii baada ya mshambuliaji wao hatari Ibrahimu Ajibu kujiunga na Mabingwa hao wa kihistoria nchini Tanzania.

“Ameongeza mkataba wa miaka miwili, ilikuwa ni baada ya kukamilisha majadiliano ambayo yalikuwa yamefikia zaidi ya asilimia 99,” kilieleza chanzo.

No comments:

Post a Comment