KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, June 18, 2017

SINGIDA UNITED YAMNASA NYOTA WA KIMATAIFA WA RWANDA


Timu ya Singida United imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Rwanda ambaye alikuwa anacheza timu ya Polisi,Danny Usengimana na kuwa mchezaji wa sita wa kigeni kusajiliwa na matajiri hao.

Mshambuliaji huyu anayetabiliwa kuwa nitishio katika kufumani nyavu ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ameingia kandarasi ya miaka miwili na kikosi cha Kocha Mkuu wa zamani wa Mabingwa Ligi Kuu ya Tanzania bara Yanga ,Hans Van Der Pluijm.

Timu ya Singida United ni timu tatu zilizopanda kushiriki Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara na nyingine ni Lipuli pamoja na Njombe Mji.

No comments:

Post a Comment