KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, June 17, 2017

HANSPOPE AMPANDIA NDEGE OKWI NA KUNASA SAINI YAKE

HATIMAYE klabu ya Simba imekamilisha mipango ya kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi.
Simba imenasa saini ya mchezaji huyo baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hanspope kufunga safari kwenda Kampala, Uganda kukamilisha mazungumzo na nyota huyo.
Okwi ni miongoni mwa wachezaji wa zamani wa Simba walioiletea mafanikio makubwa klabu hiyo katika ligi kuu ya Tanzania na michuano ya kimataifa.
Hata hivyo, bado haijawekwa wazi kuhusu kiwango cha fedha alicholipwa mshambuliaji huyo ili arejee Simba.

No comments:

Post a Comment