KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 29, 2017

NGOMA AKATA MZIZI WA FITINA, AONGEZA MKATABA WA MIAKA MIWILI YANGA



MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Zimbabwe, Donald Ngoma ametia saini mkataba mpya wa miaka miwili wa kuendelea kuichezea klabu ya Yanga.

Ngoma alirejea nchini mwanzoni mwa wiki hii huku kukiwa na taarifa kwamba, amejiunga na klabu ya Polokwane City ya Afrika Kusini kwa mkataba wa miaka mitatu.

Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya Yanga Hussein Nyika amethibitisha kumsaini mshambuliaji wa Zimbabwe Donald Ngoma kwa mkataba wa miaka miwili.

“Ngoma tumeshamsaini leo kwa mkataba wa miaka miwili kwa hiyo ataendelea kuitumikia Yanga kwa misimu miwili ijayo akiwa ni mchezaji halali wa Yanga.”

“Mashabiki wa Yanga waelewe kwamba, Ngoma bado yupo Yanga.”

Kabla ya Yanga kukata mzizi wa fitna kwa kumuongeza mkataba Ngoma, kulikuwa habari kwamba mchezaji huyo raia wa Zimbabwe huenda akatimkia Simba kwa ajili ya msimu ujao.

Ngoma aliwasili jana usiku na kupokewa na watu wa Yanga kabla ya kusaini mkataba mpya na mabingwa wa Tanzania leo Juni 29, 2017.

No comments:

Post a Comment