KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 29, 2017

OKWI ATUA TENA MSIMBAZI




MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi ametia saini mkataba wa kuichezea klabu ya Simba kwa miaka miwili.

Okwi ametia saini mkataba huo mbele ya Makamu wa Rais wa Simba, Godfrey Nyange 'Kaburu'.

Baada ya kutia saini mkataba huo, Okwi alitambulishwa kwa waandishi wa habari mbele ya mfadhili wa klabu hiyo, Mohammed Dewji.

Akizungumza wakati wa utambulisho huo, Dewji alisema usajili wa Okwi ni zawadi ya sikukuu ya Idd el Fitr kwake kwa mashabiki wa Simba.

Kwa upande wake, Okwi aliwaahidi furaha mashabiki wa Simba kwa kuwarejeshea mataji ambayo iliyapoteza kwa miaka minne mfululizo.

No comments:

Post a Comment