KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 22, 2017

UCHAGUZI RUREFA KUFANYIKA JULAI 5, 2 017


Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imetangaza kuwa Uchaguzi Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Rukwa (RUREFA), utafanyika Agosti 05, mwaka huu mjini Sumbawanga.

“Napenda kuwatangazia wadau wote wa RUREFA kuwa mchakato wa uchaguzi utaendelea kuanzia pale ulipokomea,” alisema Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF, Wakili Revocatus Kuuli mara baada ya kikao cha Kamati hiyo, kilichoketi Juni 10, mwaka huu.

Wakili Kuuli amesema uchaguzi utaendeshwa na Kamati ya Uchaguzi ya RUREFA, kwa kusimamiwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kama ilivyoanishwa kwenye taarifa ya awali.

Sasa kinachofuata ni kipindi cha kupokea na kuweka pingamizi kwa wagombea ambapo zoezi hilo litafanyika Julai 4 na 5, 2017 wakati Julai 6 na 7, mwaka huu itakuwa ni kupitia pingamizi zote na kufanya usaili wa wagombea.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa, Julai 8, mwaka huu itakuwa ni hatua ya kutangaza na kubandika kwenye mbao za matangazo matokeo ya awali ya usaili ilihali Julai 9 na 10, mwaka huu Sekretariati kuwasilisha masuala ya kimaadili kwenye kamati ya Maadili.


Kuanzia Julai 11 hadi 13, mwaka huu itakuwa ni kipindi cha kupokea na kusikiliza na kutolea maamuzi masuala ya maadili wakati Julai 14 na 15, mwaka huu ni kutangaza matokeo ya uamuzi wa Kamati ya Maadili huku Julai 16 na 17, itakuwa ni kipindi cha kukata Rufaa kwa maamuzi ya masuala ya kimaadili kwenye kamati ya rufaa ya maadili ya TFF.

Julai 18 na 19, mwaka huu itakuwa ni kipindi cha kusikiliza rufaa za kimaadili wakati Julai 20 na 21 ni kutoa uamuzi wa Rufaa huku Julai 22 na 23, ni kipindi cha kukata rufaa dhidi ya Kamati ya Uchaguzi kwenye kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya TFF.

Julai 24 hadi 26, ni kipindi cha kusikilizwa rufaa kazi itakayofanywa na Kamati ya rufaa ya Uchaguzi ya TFF ilihali Julai 27 na 28, ni kwa wagombea na kamati ya uchaguzi kujulishwa maamuzi ya Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya TFF.

Julai 29 na 30, mwaka huu ni kuchapisha orodha ya mwisho ya wagombea na kutangazwa na kubandikwa kwenye mbao za matangazo wakati kipindi cha kampeni kwa wagombea kitakuwa ni kati ya Julai 31 hadi Agosti 4, mwaka huu. Uchaguzi Mkuu wa RUREFA utakuwa Agosti 5, mwaka huu.

Hatua za awali zilizofanyika, kabla ya kusimamishwa uchaguzi kutangaza mchakato wa Uchaguzi wa TFF nafasi zinazogombewa na kubandika kwenye mbao za matangazo; kuchukua na kurudisha fomu za kuomba uongozi; hatua ya mchujo na kuchapisha na kubandika kwenye mbao za matangazo orodha ya awali ya wagombea.

No comments:

Post a Comment