KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, June 17, 2017

NENO KUTOKA KWA RAIS WA TFF KUELEKEA UCHAGUZI MKUU


Ndugu zangu viongozi, wapenzi na wadau wa mpira wa miguu Tanzania.


Kama ilivyotangazwa na kamati yetu ya uchaguzi leo tumeanza rasmi mchakato wa uchaguzi wetu.


Hiki ni kipindi muhimu kwa ustawi wa mpira wetu.


Ninaomba niwahakikishie wadau wa mpira wa miguu Tanzania kuwa Sekretarieti ya TFF ambayo kikatiba ninaisimamia mimi itaendelea na shughuli zake bila kuathiriwa na mchakato huu, hii itakuwa ni pamoja na kuandaa timu zetu mbalimbali za Taifa na kushughulikia majukumu yake mengine ya kila siku.


Aidha ninaomba niwahakikishie viongozi na wadau wa mpira wa miguu Tanzania kuwa mimi kama Rais wa TFF sina kundi katika uchaguzi huu.


Msimamo wangu ni kuwa wagombea wote wana haki sawa na sanduku la kura ndilo litaamua nani ataongoza mpira wetu kwa kipindi cha 2017-2021.


Wagombea wote ninawatakia kila la kheri na Mola awabariki na kuwaongoza.


Ahsanteni

Jamal Emil Malinzi

Rais wa TFF

No comments:

Post a Comment