KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 30, 2017

MALINZI, MWESIGWA WAPELEKWA RUMANDE HADI JULAI 3; AVEVA, KABURU HADI JULAI 13





Rais wa TFF, Jamal Malinzi hataweza kutetea kiti chake cha urais kwa kuwa amepelekwa mahabusu katika Gereza la Segerea baada ya kukosa dhamana hadi Jumatatu Julai 3 kesi yake itakaposikilizwa tena.

Malinzi pamoja na Katibu wake, Mwesigwa Celestine wanashitakiwa kwa makosa 28 yakiwemo ya kugushi na utakatishaji fedha.

Wote wawili wamepandishwa gari kwenda Segerea hadi Jumatatu kesi yao itakaposikilizwa tena.

Pamoja na wao, Rais wa Simba,  na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ wanaoshitakiwa kwa makosa ya utakatishaji, nao wamechukuliwa kupelekwa Segerea.

Kaburu na Aveva watakuwa mahabusu hadi Julai 13 baada ya kukosa dhamana kutokana na kesi inayowakabili.

Baada ya mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kuwanyima dhamana Rais wa TFF Jamal Malinzi, Katibu Mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa na afisa wa fedha Nsiande Mwanga, jopo la mawakili wa utetezi wameonekana kutoridhika na wateja wao kukosa dhamana.

“Washtakiwa kukamatwa na kufikishwa mahakamani halafu wanaomba tena upelelezi wa kesi wakati suala tayari lipo mahakamani hiyo ndio pointi kubwa ambayo tumeiibua halafu kitu kingine tulichokiibua ni pamoja na maombi ya dhamana,”  Jarome Msemwa-wakili upande wa utetezi.

“Tumeiomba mahaka itoe dhamana kwa wateja wetu, kuna sheria ya Bunge inayokataza dhamana halafu kuna katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoruhusu dhamana. Kwa hiyo kwa amri ya mahakama ambayo imesomwa leo (jana) wateja wetu wanapelekwa rumande hadi Jumatatu Julai 3, 2017.”

“Sikutarajia katika muda na wakati kama huu kutakuwa na mashitaka yanayowakabili yanayofika 28 ya aina ileile lakini ndani yake yanatengenezwa machache kufanywa ya tutakatisha fedha wakati mashitaka yote tunayaona ni kughushi na kila kitu wanacho. Mimi sikutegemea kama watasema upelelezi haujakamilika wakati uchunguzi wao wamesema ni wa muda mrefu sana,” Aloyce Komba-wakili upande wa utetezi.

“Mvutano ulikuwa ni wa kisheria ambapo mwisho wa siku mahakama ikabidi ifanye maamuzi, sisi tulikuwa tunaomba dhamana vilevile kesi ianze kusikilizwa na tulikuwa tunasema hawawezi kusema upelelezi bado haujakamilika wakati wameshakamilisha kilakitu. Vilevile tukataka mtazamo huu ubadilike hapa nchini wa kuwaleta watu mahakamani halafu uchunguzi bado haujakamilika wanaishia kukaa ndani.”

Watuhumiwa wote walikana mashitaka yote 28 yanayowakabali hivyo kesi hiyo kuahirishwa hadi Jumatatu Julai 3, 2017.

No comments:

Post a Comment