KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 15, 2015

SIMBA BINGWA KOMBE LA MAPINDUZI


TIMU kongwe ya soka ya Simba jana ilitwaa ubingwa wa michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuichapa Mtibwa Sugar kwa penalti 5-4 katika mechi ya fainali iliyopigwa kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Mshindi wa pambano hilo ilibidi apatikane kwa njia ya penalti tano tano baada ya timu hizo kumaliza dakika 90 zikiwa suluhu.
Kipa Ivo Mapunda, aliyeingia dakika za mwisho ndiye aliyeibuka shujaa wa Simba baada ya kupangua penalti ya mwisho ya Mtibwa iliyopigwa na Vicent Barnabas.
Pambano hilo lilikuwa kali na gumu kutokana na kila timu kupania kushinda ili kuibuka na ubingwa.
Katika michuano hiyo, mshambuliaji Simon Msuva aliibuka kuwa mfungaji bora baada ya kupachika wavuni mabao manne na kumpiku mshambuliaji chipukizi wa Simba, Ibrahim Hijabu, aliyefunga mabao matatu.
Kipa Saidi Mohamed wa Mtibwa Sugar aliibuka kuwa kipa bora wa michuano hiyo wakati beki Salim Mbonde wa Mtibwa Sugar aliibuka kuwa mwanasoka bora.

No comments:

Post a Comment