KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 25, 2015

MRWANDA AIBEBA YANGA, YAICHAPA POLISI MORO BAO 1-0

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

YANGA jana ilirejesha imani kwa mashabiki wake baada ya kuichapa Polisi Moro bao 1-0 katika mechi ya ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mshambuliaji Danny Mrwanda ndiye aliyeifungia Yanga bao hilo la pekee dakika ya 42, akimalizia mpira uliopanguliwa na kipa Tony Kavishe, kufuatia shuti la Simon Msuva.

Kutokana na ushindi huo, Yanga sasa imechupa nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hioyo, ikiwa na pointi 18 baada ya kucheza mechi 10. Azam inaendelea kuongoza ikiwa na pointi 20.

Katika mechi hiyo, Yanga ilicheza vizuri kipindi cha kwanza, lakini tatizo kubwa lilikuwa umaliziaji mbovu wa washambuliaji wake.

Yanga SC ilicheza vizuri kipindi cha kwanza, lakini ugonjwa wa kukosa mabao ya wazi ulijirudia kabla ya Mrwanda kuupatia tiba mwishoni mwa kipindi hicho.

Polisi ilizinduka katika kipindi cha pili na kufanya mashambulizi kadhaa kwenye lango la Yanga, ikiongozwa na Saidi Bahanuzi, lakini haikuwa na bahati ya kupata bao.

No comments:

Post a Comment