KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 18, 2015

AMAVUBI KUTUA MWANZA JAN 21


Timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi) inawasili Mwanza, Januari 21 mwaka huu kwa ajili ya mechi
ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Taifa Stars Maboresho itakayochezwa kwenye Uwanja wa CCM
Kirumba jijini humo.

Amavubi yenye msafara wa watu 26, wakiwemo wachezaji, benchi la ufundi na viongozi
itawasili kwa ndege ya RwandAir na siku hiyo hiyo jioni itafanya mazoezi kwenye Uwanja wa CCM
Kirumba. Timu hiyo itafikia kwenye hoteli ya JB Belmont.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inaingia kambini keshokutwa (Januari 18
mwaka huu), na siku inayofuata itakwenda Mwanza tayari kwa ajili ya mechi hiyo itakayofanyika
Januari 22 mwaka huu.

Kikosi hicho cha Kocha Mart Nooij ambacho ni sehemu ya maandalizi ya mechi za mchujo za
michuano ya Afrika kwa Wachezaji wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN) kinaundwa na wachezaji
26.

No comments:

Post a Comment