KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, January 5, 2015

MESSI AIPELEKA SIMBA ROBO FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI




TIMU ya soka ya Simba jana ilifuzu kucheza robo fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuichapaJKU bao 1-0 katika mchezo wa kundi C uliochezwa kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Bao pekee na la ushindi la Simba lilipachikwa wavuni na mshambuliaji machachari, Ramadhani Singano 'Messi' dakika ya 12.

Messi alifunga bao hilo kwa shuti kali la mguu wa kushoto baada ya kupokea pasi maridhawa kutoka kwa Saidi Ndemla.

Kwa matokeo hayo, Simba imetwaa uongozi wa kundi hilo ikiwa na pointi sita, ikifuatiwa na Mtibwa Sugar yenye pointi tano.

Pambano hilo lilikuwa na ushindani mkali kutokana na timu zote mbili kuonyesha soka ya kiwango cha juu, hasa katika kipindi cha pili.

Katika mechi nyingine ya kundi hilo iliyochezwa jana, Mtibwa na Mafunzo ziligawana pointi moja moja baada ya kutoka suluhu.

Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea leo wakati KCCA ya Uganda itakapomenyana na KMKM, Azam na Mtende wakati Yanga itavaana na Shaba. Mechi hizo zitaanza kuchezwa saa tisa alasiri.

No comments:

Post a Comment