KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 18, 2015

MTIBWA SUGAR YAPUNGUZWA KASI NA JKT RUVU



MTIBWA Sugar imepunguzwa kasi baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na JKT
Ruvu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Azam Complex,
Chamazi, Dar es Salaam jana.

Matokeo hayo yanairejesha Mtibwa kileleni baada ya kufikisha pointi 17, baada ya mechi tisa,
sawa na mabingwa watetezi, Azam FC, lakini timu ya Manungu inapandishwa kwa wastani wa
mabao.

JKT Ruvu imefikisha pointi 17 pia baada ya mechi 11, lakini inabaki nafasi ya tatu mbele ya vigogo
Yanga pointi 15 na Simba 12.

JKT ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya saba, mfungaji Samuel Kamuntu ambaye
aliuwahi mpira uliotemwa na kipa Said Mohammed Kasarama.

Mtibwa walifanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 36, mfungaji Ame Ally aliyemalizia kwa
kichwa kona iliyochongwa na Shijja Kichuya.

Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo jana, Coastal Union imelazimishwa sare ya bila kufungana
na Polisi Moro Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

No comments:

Post a Comment