KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, January 26, 2015

SIMBA, AZAM HAKUNA MBABE, OKWI APOTEZA FAHAMU UWANJANI


TIMU za soka za Simba na Azam jana zilishindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba ilikuwa ya kwanza kupata bao kipindi cha kwanza kupitia kwa Emmanuel Okwi kabla ya Azam kusawazisha kipindi cha pili kupitia kwa Kipre Tchetche.

Katika mechi hiyo, timu zote mbili zilicheza kwa kasi huku kila moja ikipania kutoka uwanjani na ushindi.

Wakati huo huo, mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Simba jana alipoteza fahamu uwanjani baadaya kupigwa kiwiko na mchezaji mmoja wa Azam.

Kutokana na tukio hilo, Okwi alilazimika kukimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ambako alilazwa na kuruhusiwa baada ya saa kadhaa.

Akizungumzia tukio hilo, daktari wa Simba, Salim Gembe, alisema mshambuliaji huyo amenusurika kufa.

"Okwi aligongwa kiwiko nyuma ya kichwa kwenye mishipa ya fahamu, kwa hiyo akapoteza
fahamu uwanjani. Ilikuwa mbaya sana, angeweza kupoteza maisha, lakini hali ile tuliidhibiti
wakati tunampa huduma ya kwanza uwanjani,”alisema.

“Baada ya hapo, tukaingia naye ndani kwenye zahanati ndogo ya uwanja, kuendelea kumpa tiba
hadi fahamu zikamrejea, lakini hali yake haikuwa nzuri sana, ikabidi tumkimbize Muhimbili,
ambako baada ya tiba ya takriban saa mbili, sasa yuko vizuri,”amesema Gembe.

No comments:

Post a Comment