KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 18, 2015

SIMBA, AZAM ZASHINDA LIGI KUU, YANGA YABANWA

SIMBA jana ilizoa pointi zote tatu kutoka kwa Ndanda FC baada ya kuichapa mabao 2-0 katika mechi ya ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Nangwande Sijaona mjini Mtwara.

Ushindi huo ni wa pili kwa Simba tangu ligi hiyo ilipoanza na umepokelewa kwa faraja kubwa na mashabiki wa timu hiyo baada ya kuishuhudia timu yao ikipata sare saba mfululizo na kupoteza mechi moja.

Mabao ya Simba yalifungwa na Dan Ssenkuruma dakika ya 26 aliyemalizia kwa shuti la mguu wa kushoto krosi kutoka kwa Ramadhani Singano 'Messi'.

Bao la pili lilifungwa na Elias Maguri dakika ya 68 baada ya kumalizia pasi kutoka kwa Ssenkuruma.

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo,Azam walijikita kileleni mwa ligi hiyo baada ya kuichapa Stand United bao 1-0 mjini Shinyanga.

Bao pekee na la ushindi la Azam lilifungwa na kiungo Frank Dumayo, ambaye ilikuwa mechi yake ya kwanza ya ligi kwa timu hiyo baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu.

Nayo timu kongwe ya Yanga ilishindwa kutamba mbele ya Ruvu Shooting baada ya kulazimishwa kutoka suluhu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment