KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 13, 2015

RONALDO ASHINDA TENA TUZO YA MWANASOKA BORA WA DUNIA 2014



 
 
 
 
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo,

amechaguliwa kuwa mwanasoka bora wa dunia kwa mwaka 2014.

Hii ni mara ya tatu kwa mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya Manchester United ya
England kushinda tuzo hiyo.

Mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa tuzo hiyo, Ronaldo alishangilia kwa staili ya aina
yake kabla ya kwenda kwenye kipaza sauti na kutoa hotuba ya shukurani.

" Naweza kumuona mama yangu, familia yangu. Napenda kuwashukuru wote walionipigia kura, kocha wangu, wachezaji wenzangu na rais wa klabu yangu,"alisema.

Ronaldo alishinda tuzo hiyo baada ya kupata asilimia 37.66 ya kura zilizopigwa na kumbwaga
Lionel Messi, aliyepata asilimia 15.76 na Manuel Neuer aliyepata asilimia 15.72.

Mshambuliaji huyo alikabidhiwa tuzo yake na mwanasoka nyota wa zamani wa Arsenal na
Ufaransa, Thierry Henry.

No comments:

Post a Comment