KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, December 2, 2011

Mr Ebbo afariki dunia


MWIMBAJI nguli Tanzania aliyeibuka na staili ya bongofleva kwa ‘tune’ na staili ya Kimasai, Abel Rusheraa Motika, almaarufu – Mr Ebbo amefariki dunia.
Habari za uhakika zilizoifikia blogu hii leo zinaeleza kwa, Mr. Ebbo alifariki kufuatia kusumbuliwa na ugonjwa wa kichomi kwa muda mrefu.
Amefariki akiwa nyumbani kwa familia yake, maeneo ya Usa River, Arusha.Mwanamuziki huyo alifahamika zaidi kwa nyimbo zake zenye lafudhi ya Kimasai, ikiwamo – Mi Mmasai Bwana, Kamongo na nyingine nyingi zilizoteka uwanja wa muziki.
Pia alikuwa miongoni mwa wanamuziki walioinukia kwa kufanya ‘kolabo’ na wanamuziki wengine, hasa wanaotoka Mkoa wa Tanga wakiwamo; Wagozi wa Kaya.
Mipango ya mazishi inafanywa na familia yake na huenda akapumzishwa katika mashamba ya familia yake yaliyoko Usa River.
Blogu hii inatoa pole kwa mashabiki wa muziki, marafiki, watoto, ndugu jamaa na marafiki wote wa marehemu Mr. Ebbo.

Innalilah Wainailaihi rajiuun
Bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina lake litukuzwe.

No comments:

Post a Comment