KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, December 6, 2011

BAYI ASHINDA TUZO YA MIAKA 50 YA UHURU

Filbert Bayi alivyo sasa

Filbert Bayi akiwa ameshikilia tuzo aliyoshinda enzi zake



BINGWA wa zamani wa dunia wa mbio za mita 1500, Filbert Bayi ameibuka mshindi wa tuzo ya mwanamichezo bora wa miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika baada ya kuzoa kura 13.
Upigaji kura kwa ajili ya kuwania tuzo hiyo umefanyika kupitia blogu hii ya liwazozito. Kura alizopata Bayi ni sawa na asilimia 72 ya kura zilizopigwa na wasomaji wa blogu hii.
Bayi alikuwa mwanariadha wa kwanza wa Tanzania kushinda medali ya dhahabu baada ya kushinda mbio za mita 1500 katika michezo ya Jumuia ya Madola iliyofanyika mwaka 1974 mjini Christchurch, New Zealand.
Mshindi wa pili wa mbio hizo alikuwa John Walker wa New Zealand wakati nafasi ya tatu ilinyakuliwa na Ben Jipcho wa Kenya.Bayi pia aliweka rekodi ya dunia ya mbio hizo kwa kutumia dakika 3:32:16
Mwaka 1975 Bayi alivunja rekodi ya mbio hizo iliyodumu kwa miaka minane iliyokuwa ikishikiliwa na Ryun baada ya kukimbia kwa dakika 3:51:0 mjini Kingston, Jamaica. Hata hivyo rekodi hiyo ilidumu kwa miezi michache baada ya kuvunjwa na Walker, aliyekimbia kwa dakika 3:49.4.
Bayi pia alishinda medali ya fedha katika mbio za mita 3000 kuruka vikwazo katika michezo ya Olimpiki ya mwaka 1980 iliyofanyika Moscow, Russia. Alishinda mbio hizo kwa kutumia dakika 8:12:5.
Mwanariadha huyo mkongwe pia alishinda mbio za mita 1500 katika michezo ya All Africa-Games iliyofanyika mwaka 1973 mwaka 1978 na kumbwaga Kipchoge Keino, aliyeambulia medali ya fedha.
Bayi won a silver medal in the 3000 m steeplechase at the 1980 Summer Olympics in
Moscow. He ran 8:12.5 behind Bronisław Malinowski.
Kwa sasa, Bayi ni Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) na anamiliki Taasisi ya Bayi, ambayo lengo lake kubwa ni kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana katika michezo.
Bayi pia anamiliki shule ya awali na msingi za Filbert Bayi zilizopo Kimara pamoja na shule ya sekondari iliyopo Kibaha mkoani Pwani.

Mshindi wa pili wa tuzo hiyo ni bondia Habibu Kinyogoli, ambaye alishinda medali ya fedha katika michezo ya All Africa-Games iliyofanyika mwaka 1978 nchini Nigeria.

Kinyogoli ni mmoja wa mabondia wanaoheshimika nchini kutokana na mchango mkubwa aliotoa katika ndondi za ridhaa na zile za kulipwa. Ni kocha aliyewafundisha mabondia wengi wa ndondi hizo nchini.

Kinyogoli amepata kura nne, ambazo ni sawa na asilimia 22 ya kura zilizopigwa na wasomaji wa blogu hii.

Nafasi ya tatu imechukuliwa na mwanasoka mkongwe Jella Mtagwa, aliyepata kura mbili ambazo ni sawa na asilimia 11 wakati Peter Tino ameshika mkia kwa kutoambulia kura.

Jela ni nahodha aliyeiongoza Taifa Stars kwa miaka 10 na picha yake ilikuwa kutumika katika moja ya stempu zilizotengenezwa na lililokuwa shirika la posta na simu Tanzania miaka ya 1980, lakini hakulipwa chochote. Tino ndiye mchezaji aliyeiwezesha Taifa Stars kufuzu kucheza fainali za Afrika kwa mara ya kwanza mwaka 1980 baada ya kuifungia bao la kusawazisha katika mchezo kati yake na Zambia uliofanyika mjini Ndola mwaka 1979.

Hongera sana Bayi kwa kuibuka mshindi wa tuzo hii. Blogu ya liwazozito inakutakia kila la heri katika maisha yako. Pia tunawapongeza Kinyogoli, Jella na Tino, ambao tuliwashirikisha bila ridhaa yenu, lakini kwa kutambua mchango mkubwa mlioutoa katika maendeleo ya michezo hapa nchini.

Pia tunawashukuru wale wote walioshiriki kuwapikia kura wanamichezo hawa. Mungu awabariki.

No comments:

Post a Comment