KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, February 12, 2017

SIMBA YAREJEA KILELENI LIGI KUU


SIMBA imerejea kwenye uongozi wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara kwa kishindo baada ya kuibugiza Prisons mabao 3-0 katika mechi iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo iliyoonekana kuwa ya upande mmoja, Simba ilitawala sehemu kubwa ya mchezo, hasa safu ya kiungo kutokana na Kocha Joseph Omog kuwapanga wachezaji wengi wa safu hiyo.

Iliwachukua Simba dakika 18 kuhesabu bao la kwanza lililofungwa na Juma Luizio baadaya kuunganisha wavuni krosi kutoka kwa beki Javier Bokungu.

Ibrahim Ajib aliiongezea Simba bao la pili dakika ya 28 baada ya gonga safi kati yake na Laudit Mavugo. Mabao hayo yalidumu hadi mapumziko.

Mavugo aliihakikishia Simba ushindi dakika ya 68 baada ya kufunga bao la tatu, akisindikiza wavuni krosi kutoka kwa Ajib.

No comments:

Post a Comment