KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 16, 2017

DIAMOND AKAMATWA NA POLISI, ATOZWA FAINI


MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Diamond', jana alitiwa mbaroni na kikosi cha polisi cha usalama barabarani.

Manji alifikishwa kwenye kituo hicho kwa kosa la kuendesha gari huku akiimba wimbo wake wa Marry You' huku akiwa akiachia usukani mara kwa mara, akiwa hajafunga mkanda wa gari.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye kituo hicho cha polisi, Diamond anadaiwa kutenda kosa hilo Jumamosi iliyopita, siku ambayo mwanawe wa pili wa kike alikuwa akitimiza umri wa siku 40.

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamanda Mohamed Mpinga, alikuwa miongoni mwa maofisa wa polisi walioshiriki kumuhoji msanii huyo.

Kamanda Mpinga alikiri kukamatwa kwa msanii huyo na kutiwa hatiani kwa makosa mawili, moja la kuendesha gari akiwa ameachia usukani na la pili kutofunga mkanda.

"Imebidi alipe faini kwa sababu makosa hayo mawili adhabu yake ni kulipa faini. Amelipa faini shilingi 60,000 kwa sababu kila kosa adhabu yake ni faini ya shilingi 30, 000,"alisema.

Kamanda Mpinga alisema makosa aliyokutwa nayo Diamond, yamekuwa yakifanywa na watu wengi wanapoendesha magari hivyo kukabiliwa na adhabu hizo.


No comments:

Post a Comment