KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 2, 2017

FIFA YAIAMURU YANGA KUMLIPA BRANDTS DOLA 11,000 ZA MAREKANI




Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA), limeitaka Klabu ya Young Africans ya Dar es Salaam kulipa mara moja deni la aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, Ernst Wilhelmus Johannes Brandts – Raia wa Uholanzi waliyevunja naye mkataba miaka miwili iliyopita.
Klabu ya Young Africans imetakiwa kulipa dola 11,000 za Marekani kama ambavyo iliamriwa Juni 30, 2015 na Kamati ya Hadhi ya Wachezaji ya FIFA.    
Kutolipa deni hilo kwa wakati, imetafsiriwa kwamba Yanga imevunja Kanuni ya 64 inayozungumzia Nidhamu katika FIFA yaani FDC (FIFA Disciplinary Committee).
Yanga inakabiliwa adhabu za kupigwa faini zaidi ya awali, kukatwa pointi katika Ligi Kuu ya Vodacom inayoendelea kwa sasa au kushushwa daraja.
Kamati hiyo ya Nidhamu inatarajiwa kukutana wakati wowote wiki ijayo na suala la Nidhamu ya Yanga litakuwa ajenda ili kama hawakulipa, watachukua hatua kama adhabu zinavyojieleza hapo juu
TFF imeagizwa haraka kufuatilia suala la deni hilo katika klabu ya Yanga na kurudisha majibu FIFA. TFF kupitia Katibu Mkuu, imeagizwa kupeleka barua ya FIFA katika Makao makuu ya Klabu hiyo, yaliyoko kwenye makutano ya mitaa ya Jangwani na Twiga, Dar es Salaam.
“TFF tumeliweka wazi suala hilo kama ‘Tahadhari kabla ya hatari’, kwani tungeweza kufanya mawasiliano kati ya shirikisho (TFF) na klabu (Young Africans) kwa siri tu, lakini ikitokea huko mbele klabu inakutana na adhabu mojawapo, lawama hushuka TFF kwa madai kwamba tumekalia taarifa muhimu ya kuchukuliwa hatua haraka,”imesema taarifa ya TFF leo.

No comments:

Post a Comment