KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, February 4, 2017

SIMBA YAIPUMULIA YANGA


 Timu ya Simba imekoleza mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuifanyia mauaji Majimaji kwa kuifunga mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Alikuwa Ibrahim Ajibu aliyewanyanyua mashabiki wa Simba dakika ya 19, akifunga bao kwa kichwa, akimalizia pasi ya Shiza Kichuya. Timu hizo zilikwenda mapumziko Simba ikiwa mbele kwa bao 1-0.

Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko, ambayo hata hivyo yaliisaidia zaidi Simba iliyofanikiwa kuongeza bao la pili dakika ya 64 kupitia kwa Said Ndemla.

Zikiwa zimesalia dakika mbili mchezo kumalizika, Laudit Mavugo aliiongezea Simba bao la tatu na kuifanya itofautiane kwa pointi moja na vinara wa ligi hiyo Yanga.

No comments:

Post a Comment