KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 13, 2017

YANGA YAWATEMBEZEA KICHAPO KIKALI WACOMORO


WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya soka ya klabu bingwa Afrika, Yanga jana walianza vyema michuano hiyo baada ya kuitandika Ngaya FC ya Comoro mabao 5-1 mjini Coron.

Wafungaji wa mabao ya Yanga walikuwa Justin Zullu, Amis Tambwe, Juma Mahadhi, Simon Msuva na Obrey Chirwa.

Kutokana na ushindi huo, Yanga sasa inahitaji sare ya aina yoyote katika mechi ya marudiano ili iweze kusonga mbele katika michuano hiyo.

Timu mbili hizo zinatarajiwa kurudiana Jumamosi ijayo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment