KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, February 26, 2017

STEVE NYERERE ALIPUA BOMU, ASEMA HAKUNA MSANII ANAYEIDAI CCM


MSANII wa maigizo nchini Steven Mangele (Steven Nyerere), amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM), ni sawa na bahari, haiwezi kuyumba kwa kuondoka kwa msanii Wema Sepetu, lakini amesikitishwa na kujitoa kwake kutumia kwa uongo kuwa anakidai Chama.

Amesema jitihada zake za kumnusuru Wema, asijiunge na chama kisichoeleweka, zimemsababishia matatizo kutokana na sauti ya maridhiano kati yake na Mama, Mariam Sepetu, kumchonganisha na wanasiasa.

Steve alisema mama yake Wema, mbali na kumuharibia maisha, amejivua nguo kama mzazi aliyeaminika katika jamii na kumtaka Wema kukumbuka mazuri ya CCM, badala ya kusema uongo, kwa kuwa wasanii wote waliokuwa katika kampeni na Chama, walilipwa na kumaliza mkataba wao.

Akizungumza jana, jijini Dar es Salaam, Steve alikiri sauti iliyosambaa katika mitandao ya kijamii ni yake na alitumia mbinu za propaganda na usanii kueleza uongo na kuwasingizia viongozi mbalimbali ili kumridhisha mama Wema ili ashughulikie tatizo la mwanawe bila ya jazba.

Alisema CCM ni kama bahari na ndio maana wametoka vigogo nguli, lakini
Chama hakikuyumba na wapo waliowahi kuwa viongozi wakuu, wameshitakiwa na kuhukumiwa, lakini hawakurudisha kadi za chama hivyo ni vyema Wema angejitathimini.

“Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda anayo haki ya kusafisha mji wake kwani ndiye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama. Katika majina ya walengwa, alitajwa dada yangu, swahiba wangu, rafiki yangu kipenzi Wema Sepetu na mtu wa kwanza kupigiwa nilikuwa mimi,”alisema.

Alisema hana mamlaka na uwezo wa kuwafikia viongozi wakuu
na pia hakuweza kusema jambo hilo jema au sio jema, lakini alikuwa akiangalia upande wa mwenzake aliyekata waliyekata kuni pamoja, akiamini wataota moto pamoja.

Steve alisema alishangaa kuanza kupokea simu za vitisho kuwa yeye ndiye anayetoa majina wakati hakuwepo Dar es Salaam, alikuwa Mwanza na kabla ya kurekodiwa, mama Wema alimpigia simu mara kwa mara na kumuahidi kama mzazi kuwa, yote hayo yanawezekana na yataisha.

“Lakini tena zikaanza simu za kunitukana kuwa nimemkimbia Wema akiwa ndani siku ya tatu na mama kuanza kunitisha kuwa atanifanya kitu kibaya na Wema atahama chama. Nilimuamini mama huyo ni mzazi bila kuwa na  shaka  na nikatumia sifa za chama changu kutetea chama na kutumia sanaa kumridhisha mzazi wangu na hili lilifanyika siku tano kabla, sasa kwa nini itolewe wakati huu,"alihoji.

Steve alisema wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka juzi, wasanii wote walioshiriki walilipwa vizuri na kama yupo ambaye hakulipwa, ajitokeze. Alisema Wema ndiye aliyelipwa vizuri zaidi kwa kuwa alikuwa makamu mwenyekiti wa wasanii.

"Tulijitosa kwenye kampeni sisi wenyewe. Tuliifuata CCM na kuiomba tushiriki kwenye kampeni, sio kwamba wao ndio waliotufuata na wazo hilo nililitoa mimi. Hakuna msanii anayeidai CCM tusichume dhambi bure,"alisisitiza.

No comments:

Post a Comment