KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, February 21, 2017

SERIKALI YAZIONYA SIMBA NA YANGA


Ndugu Watanzania Jumamosi, tarehe 25/02/2017 saa 10.00 jioni Uwanja wa Taifa tutakuwa na mchezo mkubwa wa kati ya Simba SC na Yanga FC.

Ikumbukwe kuwa mchezo uliopita wa timu hizi uliochezwa kwenye uwanja huu tarehe 1/10/2016 zilitokea vurumai zilizosababisha Serikali kuufungia Uwanja kwa zaidi ya miezi mitatu.Vurugu hizo zilisababisha uharibifu wa miundombinu ikiwemo uvunjifu wa viti,mageti na mbaya zaidi baadhi ya watu walijerehuliwa.

Tunaomba waandishi na wadau wote tushirikiane kuelimisha umma wa wapenda michezo kuwa Michezo ni Furaha, Amani na Upendo.

Kuelekea mchezo ujao tungependa kueleza yafuatayo:-

Tunawaomba wadau wote tujenge utamaduni wa kununua tiketi mapema kwani mpaka sasa tiketi zinapatikana kupitia SELCOM. Hii itaondoa msongamano na lawama zisizo za lazima.

Tunafahamu kuwa kuna changamoto za matumizi ya mfumo wa Ki- elektroniki lakini hatuna budi kuendelea kuelimishana na kujifunza kwani huko ndiko Dunia ilipo,tutakua watu wa ajabu leo tukisema hatuwezi kutumia mfumo huu kisa changamoto hizi ndogondogo zinazojitokeza.

Tujiepushe na vurugu za aina yoyote siku ya mchezo kwani Serikali haitamvumilia mtu yeyote atakayepelekea uvunjifu wa amani siku ya mchezo.

Kutakua na ulinzi wa kutosha ndani na nje ya Uwanja hasa ukichukulia kuwa kuna kamera zenye uwezo wa kumuona kila mtu anayeingia Uwanjani na kila anachokifanya.Tutapiga picha na kuzirusha kwenye TV kubwa ya Uwanja kwa wale wote watakaobainika kuashiria/kutenda vurugu sheria itachukua mkondo wake.

Tunatoa rai kwa waamuzi waliopewa dhamana ya kuchezesha mchezo huu,wajue kuwa wana dhamana kubwa hivyo ni vyema wakafuata kanuni na sheria za mchezo husika ili kuepusha malalamiko.

Mwisho napenda niwatakie mchezo mwema kwa timu zote wajue kuwa Watanzania wanategemea burudani nzuri kutoka kwao,na niwaombe mashabiki wakumbuke kuwa wajibu wao mkuu ni kuzishangilia na kuzipa hamasa timu zao na si vinginevyo.

No comments:

Post a Comment