KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, February 15, 2017

MALINZI AIPONGEZA LIPULI KUPANDA DARAJA



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameuandikia barua uongozi wa Lipuli ya Iringa kwa mafanikio ya kupanda daraja msimu huu kutoka Ligi Daraja la Kwanza hadi Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimuwa 2017/18.

Lipuli ya Iringa imepanda daraja baada ya kupita miaka 17 na Rais Malinzi amesema katika barua yake hiyo kwenda kwa Katibu Mkuu wa Lipuli, akisema: “Nitumie fursa hii kukupongeza wewe, uongozi wa klabuy ako, benchi la ufundi na wadau wote wa timu ya Lipuli kufuatia kupanda daraja kwenda Ligi Kuu.

“Bila shaka ni kazi kubwa imefanyika ikihusisha kujitolea kwa ari na mali kuhakikisha mnafika hapa mlipo,” ilisema barua hiyo na kuongeza: “Rai yangu kwenu ni kuongeza juhudi na kuendesha klabu kwa weledi mkubwa zaidi ili muweze kuwa washindani wa kweli katikal igi.”

Lipuli iliyo kuwa kundi “A” imepanda daraja na kuzipiku timu zaK iluvya United ya Pwani, Pamba ya Mwanza, African  Sports yaTanga, Polisi Dar, Ashanti United, Friends Rangers, Mshikamano za Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment