KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 3, 2011

Warembo Miss Tanzania kambini J'Tatu


WASHIRIKI wa shindano la kumsaka mrembo wa Tanzania, Vodacom Miss Tanzania 2011 wanatarajiwa kuingia kambini Agosti 8 mwaka huu.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino Agency International, inayoratibu mashindano hayo, Hashim Lundenga, alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, warembo 30 wanatarajiwa kuwania taji hilo.
Lundenga alisema warembo hao walipatikana baada ya kufanya vizuri katika ngazi ya wilaya, mikoa na kanda. Alisema jumla ya kanda kumi na moja zilishirikishwa katika hatua hiyo.
Kwa mujibu wa Lundenga, kambi ya warembo hao itakuwa katika Jiji la Dar es Salaam, lakini hakutaja hoteli watakayoishi. Aliwataka washiriki wote kuripoti kwenye ofisi za Miss Tanzania zilizopo mtaa wa Mkwepu kuanzia saa nne asubuhi.
Lundenga alisema, iwapo itatokea mshiriki kushindwa kufika kwa wakati na tarehe iliyotajwa hapo juu, atakuwa amejiondoa mwenyewe katika mashindano hayo na nafasi yake kupewa mshiriki mwingine. Aliwataja warembo waliopata tiketi ya kushiriki kwenye shindano hilo kuwa ni Chiaru Masonobo (Dares Salaam), Zerulia Manoko, Maua Kimambo, Dalilah Ghalib, Christine Mwenegoha (kanda ya kati), Chritine William, Atu Daniel, Leyla Juma (nyanja za juu kusini), Zubeda Seif, Stacey Alfred, Rose Hubert (kanda ya kaskazini).
Washiriki wengine ni Husna Twalib, Cynthia Kimasha, Mwajab Juma (kanda ya Temeke), Neema Mtitu, Weirungu David (open university), Glory Lory, Blessing Ngowi (higher learning), Loveness Flavian, Asha Salehe, Mariaclara Mathayo, (kanda ya mashariki), Trace Sospeter, Irene Karugaba, Glory Samwel (kanda ya ziwa), Stella Mbuge, Husna Maulid, Hamisa Hussein (kanda ya Kinondoni), Salha Israel, Alexia Willims, Jenifer Kakolaki (Ilala).
Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania, George Rwehumbiza alisema, kampuni yake ipo tayari kuwapokea warembo kwani mwaka huu wamejiandaa vya kutosha na wanatarajia kuyafanya mashindano hayo kuwa ya kimataifa zaidi.
Rwehumbiza alisema kauli mbio ya mashindano ya mwaka huu ni 'Kazi ni kwako'.

No comments:

Post a Comment