KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 11, 2011

Ndoa ilinishinda-Aunt Ezekiel


MWIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Aunt Ezekiel amesema aliwahi kuolewa, lakini ndoa ilimshinda baada ya mume wake kurudi nyumbani akiwa amevaa kondomu.
Akizungumza wiki iliyopita katika kipindi cha luninga ya Clouds, kinachoendeshwa na Zamaradi Mketema, msanii huyo alisema alishituka baada ya kumuona mumewe amevaa mpira huo wa kiume.
Aunt Ezekiel alisema, hakutegemea kama angemkuta mume wake na mpira huo na baada ya hapo, alibeba kilicho chake na kuitema ndoa yake.
"Siku hiyo mume wangu alirudi asubuhi akiwa hajavua kondomu aliyokuwa ametoka kuitumia. Nilishindwa kuvumilia, nikaondoka," alisema Aunt Ezekiel, ambaye aliwahi kuzaa mtoto, akafariki dunia.
Msanii huyo aliyezaliwa mwaka 1986 jijini Dar es Salaam, akiwa ni mtoto wa mwanasoka, aliyewahi kutamba nchini katika miaka ya 1970 hadi 1980, Ezekiel Greyson pia, alikiri kuwa anapenda fedha na si mabwana wenye nazo kama inavyoelezwa.
"Sijui kama kuna mtu hataki pesa, hata wewe (Zamaradi) naona unataka pesa na mimi pia nazitafuta," alisema.
Mcheza filamu huyo mwenye mvuto aliongeza kuwa, hata mabwana wenye fedha, ni wao wanaomfuata, si kwamba yeye anajilengesha kwao kwa ajili ya kutaka pesa.
Katika kipindi hicho, Aunt Ezekiel alizungumzia mengi katika maisha yake ya filamu, ikiwa ni pamoja na kukiri kwamba, aliwahi kumchapa makonde msichana mmoja, aliyetumwa kumvamia kwa madai ya kutembea na bwana wa mtu.
"Yule msichana baada ya kunivamia, sikumlazia damu, nilimchangamkia na baada ya kumfikisha polisi, alisema alitumwa na dada mmoja aje kunivamia kwa madai namchukulia bwana wake," alisema.
Hata hivyo, hakutaja jina la mwanamke aliyepigana naye wala aliyemtuma na kusisitiza kuwa, hatembei na huyo mwanaume kama inavyodaiwa.

No comments:

Post a Comment