KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 11, 2011

Mwajabu awa Vodacom Miss Top Model 2011



MREMBO Mwajabu Juma, ametwaa taji la 'Miss Top Model' katika shindano lililofanyika juzi usiku katika Hoteli ya Giraffe mjini Dar es Salaam.
Katika shindano hilo lililowashirikisha warembo 30 wanaowania taji la Vodacom Miss Tanzania 2011, Mwajabu alipata kura nyingi kutoka kwa majaji.
Majaji hao Asia Idarous, Kisa Zimba na Mariam Hashim walimpa pointi nyingi mshiriki huyo kutokana na kuonekana kuwa na vigezo vyote vinavyostahili kwa mwanamitindo na kuwabwaga wenzake walioingia hatua ya tano bora.
Warembo hao, kanda wanazotoka zikiwa kwenye mabano ni Jenifer Kakolaki (Ilala), Cynthia Kimasha (Temeke), Alexia Williams (Ilala) na Zerulia Manoko (Kanda ya Kati).
Kutokana na matokeo hayo, warembo hao wamekata tiketi ya kuingia moja kwa moja katika hatua ya 15 bora ya shindano hilo.
Akizungumza jana, Mkurugenzi wa Kamati ya Vodacom Miss Tanzania, Hashim Lundenga, alisema mfumo wa kumpata mshindi mwaka huu umebadilika na ni lazima washiriki washinde mataji madogo madogo ili waingine katika fainali.
Lundenga alisema kutokana na mabadiliko hayo, warembo 15 pekee ndio watakaoingia katika hatua ya 15 bora baada ya kupatikana katika mataji mengine. Aliyataja mataji hayo kuwa ni la kipaji, mvuto wa picha, michezo na mwonekano halisi, ambapo kila taji litatoa washindi watano.
Alisema warembo wengine, ambao hawatashinda mataji hayo, hawatapata nafasi ya kuingia katika hatua ya 15 bora, ambayo warembo wake watawania nafasi ya kuingia 10 bora, tano bora na hatimaye kumpata mshindi.
Warembo wanaoshiriki shindano hilo na kanda wanazotoka katika mabano ni Jenifer Kakolaki (Ilala), Leyla Juma (Nyanda za Juu Kusini), Mwajabu Juma (Temeke), Mariaclara Mathayo (Kanda ya Mashariki), Cythia Kimasha (Temeke), Christine William (Nyanda za Juu Kusini), Hamisa Hassan (Kinondoni), Alexia Williams (Ilala), Stacy Alfred (Kanda ya Kaskazini), Asha Salehe (Kanda ya Mashariki), Zubeda Seif na Rose Hubert (Kanda ya Kaskazini), Maua Kimambo (Kanda ya Kati) na Grolr Samuel (Kanda ya Ziwa).
Wengine ni Neema Mtitu (Chuo Kikuu Huria), Atu Daniel (Nyanda za Juu Kusini), Blessing Ngowi (Elimu ya Juu), Weirungu David (Chuo Kikuu Huria), Chiaru Masonobo (Chuo Kikuu DSM), Irene Karugaba (Kanda ya Ziwa), Delilah Gharib (Kanda ya Kati), Tracy Sosppeter (Kanda ya Ziwa), Husna Twalib (Temeke), Loveness Flavian (Kanda ya Mashariki), Christine Mwegoha (Kanda ya Kati), Husna Maulid (Kinondoni), Zerulia Manoko (Kanda ya Kati), Salha Israel (Ilala), Groly Lory (Vyuo Vikuu) na Stella Mbuge (Kinondoni).

No comments:

Post a Comment