KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 11, 2017

YANGA YAZINDUKIA NJOMBE




Mabingwa Watetezi Wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania bara baada ya kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji Njombe Mji ,Mchezo uliopigwa katika uwanja wa Saba Saba uliopo Mjini Njombe.

Mshambuliaji hatari wa Zamani wa Simba,Ibrahim Ajibu Migomba aliwanyanyua mashabiki wa Yanga baada ya kufunga goli maridadi kunako dakika ya 16 kwa shuti la Faulo ambalo sawa na umbali wa mita 30 lililoenda moja kwa moja na kumuacha Mlinda Mlango wa Njombe Mji hana la kufanya.

Huu ni ushindi wa kwanza kwa George Lwandamina msimu mpya wa Ligi baada ya mchezo wa kwanza kulazimishwa sare ya kufungana goli 1-1 dhidi ya Lipuli Fc mchezo ambao ulipigwa uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Yanga waliongeza kasi ya mashambulizi baada ya bao hilo, lakini hawakuwa na bahati ya kufunga zaidi kutokana na kushindwa kutumia vizuri nafasi walizotengeneza.
 
Yanga  walitawala vizuri mchezo kipindi chote cha kwanza na wangeweza kuvuna mabao zaidi kama wangekuwa makini katika utumiaji wa nafasi ambazo walizipata
 
Kipindi cha pili kilibadilika kidogo na vijana wa Hassan Banyai wakaanza kuwavimbia mabingwa watetezi wa Ligi Kuu walio chini ya kocha Mzambia, George Lwandamina.
 
Sifa zimuendee kipa Mcameroon wa Yanga, Youthe Rostand aliyeokoa michomo mingi ya hatari kipindi hicho cha pili na kuinusuru timu yake kufungwa.
 
Katika kipindi hicho, beki wa Njombe Mji, Remmy Mbuligwe alikimbizwa hospitali baada ya kuumia kufuatia kugongana na beki wa Yanga Juma Abdul.

Awali ya hapo, Yanga nayo ilipata pigo baada ya kiungo wake Mzimbabwe, Thabani Kamusoko kuumia na kushindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Raphael Daudi dakika ya 49.   
 
Katika mechi nyingine za leo; Lipuli FC imeilaza 1- 0 Stand United, Mbeya City imefungwa nyumbani 1-0 na Ndanda FC, Singida United imeifunga 2-1 Mbao FC, Kagera Sugar imelazimishwa sare ya 1-1 Ruvu Shooting, Mtibwa Sugar imeshinda 1-0 dhidi ya FC Mwadui.

Kikosi cha Njombe Mji kilikuwa; David Kisu, Agaton Mapunda, Remmy Mbuligwe, Laban Kamboole, Peter Mwangosi, Joshua John, Awadh Salum, Hassan Kapalata/Behewa Sembwana dk80, Notikeli Masasi, Ditrim Nchimbi na David Nakpa/Raphael Siame dk47.

Yanga SC; Youthe Rostand, Juma Abdul, Gardiel Michael, Andrew Vincent, Kevin Yondan, Papy Kabamba Tshishimbi, Juma Mahadhi, Thabani Kamusoko/Raphael Daudi dk49, Donald Ngoma/Obrey Chirwa dk56, Ibrahim Hajib na Emmanuel Martin/Yussuf Mhilu dk70.

No comments:

Post a Comment