KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 22, 2017

SIMBA YAVUTWA MKIA NA MBAO FC


TIMU kongwe ya soka ya Simba jana ilishindwa kuendeleza ubabe baada ya kulazimishwa kutoka sare ya mabao 2-2 na Mbao FC katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Simba itabidi ijilaumu kwa kushindwa kutoka uwanjani na ushindi, kwani iliweza kuwa mbele ya Mbao mara mbili, lakini wapinzani wao hao waliweza kusawazisha.

Wakongwe hao wa soka nchini waliuanza mchezo huo kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kwanza dakika ya 16 kupitia kwa Shiza Kichuya, aliyeunganisha wavuni kwa kichwa krosi kutoka kwa beki Erasto Nyoni. Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.

Mbao ilipata bao la kusawazisha dakika ya 46 kupitia kwa Habibu Kondo kwa shuti kali la mbali lililompita kipa Aishi Manula na mpira kujaa wavuni.

Dakika tatu baadaye, Simba iliongeza bao la pili lililofungwa na James Kotei, aliyeunganisha wavuni mpira wa adhabu uliopigwa na Nyoni baada ya Haruna Niyonzima kuchezewa rafu.

Zikiwa zimesalia dakika tisa pambano hilo kumalizika, Mbao ilisawazisha kwa bao lililofungwa na Boniface Maganga, akiwa nje kidogo ya eneo la hatari.

No comments:

Post a Comment