KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 18, 2017

YANGA YABANWA MBAVU NA MAJIMAJI


Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania timu ya Yanga wameshindwa kutamba kwenye uwanja wa Maji Maji Mjini Songea baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na wenyeji wana rizombe MajiMaji.

Mpira ulianza kwa kasi huku Yanga wakionekana kulishambulia lango la MajiMaji kama washambuliaji akina Ngoma,Ajib pamoja na Chirwa wangekuwa makini wangetoka kipindi cha pili na bao hadi mapumziko timu zote zilikwenda sare ya bila kufungana.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko na MajiMaji waliongeza umakini na kulishambulia lango la Yanga kama Nyuki na kunako dakika ya 54 Mshambuliaji wa zamani wa Mbeya City Peter Mapunda aliwanyanyua mashabiki wa Maji Maji baada ya kufunga goli safi kwa kumzidi maaarifa beki kisiki wa Yanga Kelvin Yondani.

Kuingia kwa bao hili liliwachanga Mabingwa hao watetezi na kuanza kuliandama lango la Maji Maji dakika ya 81 Mshambuliaji wa Kimataifa Donald Dombo Ngoma aliisawazishia bao Yanga kwa kichwa akipokea krosi ya Obrey Chirwa na kumuacha Mlinda Mlango wa Zamani wa Simba,Andrew Ntalla akiruka bila majibu.

Dakika ya 84 Yanga walipata pigo baada ya winga wao hatari , Emmanuel Martin aliumia na kukimbizwa hospitali  baada ya kugongana na mchezaji wa Maji Maji, Marcel Kaheza.

Hadi Mwamuzi anamaliza Mpira timu zote zimeweza kugawana pointi moja moja na kwa matokeo hayo Yanga wamefikisha alama tano wakiwa wamecheza mechi tatu na wanatarajia kurudi jijini Dar es salaam baada ya kucheza mechi mbili ugenini na watakuja kuvaana na timu ya Mtibwa Sugar ya Morogoro kwenye uwanja wa Uhuru.

No comments:

Post a Comment