KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 25, 2017

TFF YAINGIA MKATABA NA KCB



Shirikisho la soka nchini TFF, leo Septemba 25 limesaini mkataba na benki ya KCB wenye thamani ya shilingi 325,000,000.

Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo Rais wa TFF Wallace Karia amesema huo ni ushahidi kuwa shirikisho lina ushirikiano na wadau mbalimbali wa mpira nchini.

Aidha Karia amesema fedha hizo zitaelekezwa kwenye kukuza vipaji vya soka pamoja na maendeleo ya soka nchini kwa ujumla.

Huu ni mkataba mkubwa wa kwanza kusainiwa na shirikisho hilo tangu uongozi mpya chini ya Rais Wallace Karia ulioingia madarakani August 12 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment