KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 18, 2017

SIMBA YAIBAMIZA MWADUI MABAO 3-0



Mshambuliaji wa kimataifa kutoka Uganda Emmanuel Okwi ameendelea kuweka rekodi yake baada ya kufunga magoli mawili wakati Simba ikiilaza Mwadui FC jumla ya magoli 3-0 Mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Uhuru maarufu kama Shamba la bibi jijini Dar es salaam.

Okwi amecheza mechi mbili akiwa na Simba na tayari amefikisha jumla ya magoli 6 baada ya ufunguzi kufunga magoli 4 wakati Simba ilipoidungua Ruvu Shooting jumla ya magoli 7-0 yaani wiki.
 

Okwi alianza kuwanyanyua mashabiki wa Simba dakika ya saba baada ya kupokea pokwiasi toka kwa winga Shiza Kichuya na kupiga shuti la mita 20 na kumuacha hoi Golikipa wa Mwadui,Arnold Massawe ambaye alionekana kutokuwa makini mara nyingi alikuwa anatoka toka golini.
 

Mwadui pamoja na kumiliki vizuri mpira walipopata nafasi, lakini hawakuwa na mipango kabisa ya kuipenya ngome imara ya Simba chini ya mabeki wa timu za taifa za Uganda na Tanzania, Juuko Murshid na Salim Mbonde hadi mapumziko Simba walikuwa mbele kwa goli 1-0.
 

Kipindi cha pili nyota ya Simba iliendelea kung’ara na dakika ya 67, Okwi tena akawainua vitini mashabiki wa Wekundu wa Msimbazi kwa kufunga la pili kwa shuti la umbali wa mita zisizopungua 20 baada ya pasi ya beki Mohammed Hussein ‘Tshabalala’.
 

Mashabiki wa Simba walizomea mabadiliko yaliyofanywa na kocha Mcamroon, Joseph Marius Omog mara mbili kwanza akimtoa Mghana Nicholaus Gyan na kumuingiza Mwinyi Kazimoto dakika ya 61 na baadaye akimtoa Kichuya na kumuingiza Mrundi, Laudit Mavugo dakika ya 65 wakionekana kabisa kutaka mshambuliaji John Bocco ndiye atolewe.
 

Bocco akawaonyesha mashabiki wa Simba kwamba Omog alikuwa sahihi katika mabadiliko yake kwa kufunga bao la tatu dakika ya 72 kwa shuti la umbali wa mita 20 na zaidi pia.
 

Baada ya kucheza mechi tatu wakiwa jijini Dar es salaam wekundu wa Msimbazi Simba  watasafri kwenda kanda ya Ziwa ambapo watacheza mechi mbili ya kwanza watacheza kwenye uwanja wa CCM Kirumba na wenyeji timu ya Mbao FC na baadaye wakwenda mkoani Shinyanga kucheza na Stand United.

No comments:

Post a Comment