KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 8, 2017

TAARIFA KUHUSU WA WAAMUZI TANZANIA


Kamati ya Utendaji ya Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) ilikuwa na kikao chake cha kwanza kilichofanyika Julai 6, 2017 hapa jijini Dar es Salaam.
 
Mambo muhimu yafuatayo yalitolewa uamuzi.


1. Kumpongeza Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Bw. Wallace Karia na Makamu wa Rais, Bw. Michael Wambura pamoja na Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji ya TFF kwa kuchaguliwa kwao.


2. Tumesimamisha kozi zote kwa waamuzi wapya kuanzia Septemba 7, mwaka huu. Mitihani iliyokwishafanywa kabla ya Septemba 7, mwaka huu ni halali na itumwe kwa Katibu Mkuu wa FRAT - Taifa mara moja ikiambatanishwa na ada zake.


3. Makatibu wote wa FRAT - Mkoa kwa mikoa yote ya Tanzania Bara wakumbushwe majukumu yao kwani inaonekana ni kama wamepitiwa ikiwa ni pamoja na kutuma kwa Katibu Mkuu FRAT - Taifa orodha ya waamuzi wote wa madaraja yote walio hai kwa kuchezesha na walio hai kiuanachama.


4. Tumekumbusha waamuzi kuwa na darasa la mara moja kwa wiki lijulikanalo kama ‘Sunday Class’ madarasa hayo yawe kila Makao Makuu ya Mkoa na Makao Makuu ya Wilaya.


5. Tumekubaliana uchaguzi mdogo ufanyike wakati wa mapumziko ya ligi ya wiki mbili za mwezi Januari. Tayari tumewasiliana na na Kamati ya Uchaguzi.


6. Kuwaleta pamoja waamuzi (wanachama) wote nchini bila kujali umri.


7. Kuendelea kuzalisha waamuzi wapya toka kwenye shule za sekondari, vyuo na nje ya shule za sekondari na vyuo kwa wenye sifa.


8. Kuboresha mafunzo na upandaji wa madaraja kwa waamuzi wenye madaraja.


9. Kukemea na Kupambana na rushwa kwa waamuzi hadharani kwa kushirikiana na TFF na Takukuru.


10. Kutetea kwa nguvu zote haki za waamuzi.


11. Kuboresha mawasiliano kwa ngazi zote na kwa mwanachama ye yote.


12. FRAT kiwe chama cha mfano kwa wanachama wake kwa kuwa na maadili mema, yanayompendeza Mungu.


13. Misingi kumi ya “FIFA FAIR PLAY” ni msingi wa maendeleo ya mwamuzi.


14. Wote kwa pamoja tukatae rushwa na tuiangamize rushwa kwa maendeleo ya mpira wetu.

No comments:

Post a Comment