KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, August 6, 2016

KILA LA HERI SERENGETI BOYS LEO

TIMU ya soka ya taifa ya vijana wa chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys leo inajitupa dimbani kumenyana na timu ya vijana wa umri huo ya Afrika Kusini.

Pambano hilo limepangwa kuanza saa 9 alasiri kwa saa za Afrika Kusini, sawa na saa 10 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas, aliyefuatana na timu hiyo nchini Afrika Kusini, amesema mapema leo asubuhi kuwa, vijana wamejiandaa vyema kwa mechi hiyo na wanauhakika mkubwa wa kuibuka na ushindi.

No comments:

Post a Comment