KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, August 31, 2014

SIMBA YAIPIGA KMKM 5-0


TIMU kongwe ya soka nchini, Simba jana usiku iliibugiza KMKM mabao 5-0 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.


Katika mechi hiyo, Kocha Patrick Phiri wa Simba aliendelea kukitumia kikosi kile kile, ambacho kimecheza mechi tatu za kirafiki mjini hapa.

Kipigo hicho ni cha pili mfululizo kwa KMKM. Jumatano ya wiki iliyopita, KMKM ilipigwa mabao 2-0 na Yanga kwenye uwanja huo.

Mshambuliaji Hamisi Tambwe aliendelea kudhihirisha kuwa ni tishio katika kuzifumania nyavu baada ya kuifungia Simba mabao mawili kati ya matano. Mabao mengine yalifungwa na Amri Kiemba, Ramadhani Singano na Elius Maguri.

Kocha Phiri alilazimika kubadili kikosi chake chote cha kwanza na kuingiza wachezaji wengine katika kipindi cha pili.

Katika mechi hiyo, Emmanuel Okwi, ambaye usajili wake umezua utata, alijikuta akisugua benchi kama ilivyokuwa kwa beki Donald Musoti, ambaye amechwa kwa vile ana mipangoa ya kwenda Arabuni.

Viongozi kadhaa wa Simba, wakiwemo wanaounda kundi la Marafiki wa Simba, walikuwepo uwanjani kushuhudia mechi hiyo.

No comments:

Post a Comment