KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 21, 2014

SIMBA, YANGA KUVAANA OKTOBA 12 LIGI KUU


Add caption


MIAMBA ya soka nchini, Simba na Yanga inatarajiwa kushuka dimbani Oktoba 12 mwaka huu katika mechi ya mzunguko wa kwanza wa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara.

Ratiba ya ligi hiyo iliyotolewa jana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), inaonyesha kuwa mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa ratiba, miamba hiyo ya soka inatarajiwa kurudiana Februani 2015 katika mechi ya mzunguko wa pili itakayochezwa kwenye uwanja huo.

Michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara imepangwa kuanza Septemba 20 mwaka huu, ikitanguliwa na mechi ya kuwania Ngao ya Jamii kati ya mabingwa watetezi, Azam na Yanga zitakazomenyana Septemba 12 mwaka huu.

Katika mechi za ufunguzi wa ligi hiyo, Azam itamenyana na Polisi Moro kwenye Uwanja wa Azam Complex, Mtibwa Sugar itaikaribisha Yanga kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, Stand United itavaana na Ndanda FC mjini Shinyanga, Mgambo JKT na Kagera Sugar mjini Tanga, Ruvu Shooting na Prisons mjini Pwani, Mbeya City na JKT Ruvu mjini Mbeya, Simba na Coastal Union mjini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment