KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, August 15, 2014

MWAMEJA, NSAJIGWA, PAWASA, LUNYAMILA KUUNDA KIKOSI CHA TANZANIA ALL STARS KITAKACHOMENYANA NA REAL MADRID






 NYOTA kadhaa maarufu wa zamani wa soka nchini, wameitwa kwenye kikosi cha Tanzania All Stars Veterans, kitakachomenyana na wanasoka wa zamani wa klabu ya Real Madrid ya Hispania.

Pambano hilo la aina yake na linalosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka nchini, limepangwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Miongoni mwa nyota hao ni makipa Mwameja Mohamed na Manyika Peter na mebeki Nsajigwa Shadrack, Mecky Mexime, Boniface Pawasa, John Mwansasu, Abubakar Kombo, George Masatu na Habib Kondo.

Viungo ni Suleiman Matola, Shaaban Ramadhani, Salvatory Edward, Sabri Ramadhani ‘China’, Yussuf Macho, Abdul Mashine, Abdul Maneno, Mao Mkami, Steven Nyenge, Madaraka Suleiman, Akida Makunda na Mtwa Kihwelo.

Washambuliaji ni Monja Liseki, Iddi Moshi, Dua Said, Emmanuel Gabriel, Said Maulid, Thomas Kipese, Nasor Mwinyi ‘Bwanga’, Edibilly Lunyamila, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’, Clement Kahabuka, Madaraka Suleiman na Akida Makunda.

Kikosi hicho kitakuwa chini ya makocha Charles Boniface Mkwasa na wasaidizi wake ni Freddy Felix Minziro na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’. Daktari wa timu hiyo atakuwa Mwanandi Mwankemwa na viongozi ni Mtemi Ramadhani, Hassan Mnyenye, Omar Gumbo na Hamisi Kisiwa.

Kikosi cha Real Madrid kilichosheheni nyota mbalimbali waliowahi kung'ara katika ligi kuu ya Hispania, kinatarajiwa kutua nchini Agosti 22 mwaka huu, kikiwa na kina Luis Figo, Zinedine Zidane, Claude Makelele na wengine.

Mbali na kucheza mechi hiyo ya kirafiki, kikosi hicho kinatarajiwa kufanya ziara ya kiutalii katika vivutio mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kupanda Mlima Kilimanjaro.

Real Madrid inakuja nchini kwa mwaliko wa Kampuni ya Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), chini ya Mkurugenzi wake Mkuu, Farough Baghozah.

No comments:

Post a Comment