KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 13, 2014

REAL MADRID BINGWA KOMBE LA SUPER


MABAO yaliyofungwa na mwanasoka bora wa dunia, Cristiano Ronaldo juzi yaliiwezesha Real Madrid kutwaa Kombe la Super la Ulaya baada ya kuichapa Sevilla mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Cardiff City.

Ronaldo alifunga bao la kwanza dakika ya 30 kabla ya kuongeza la pili dakika ya 49 kutokana na pasi maridhawa kutoka kwa Gareth Bale, aliyekuwa akicheza kwenye ardhi ya nyumbani.

Wakati huo huo, Chelsea juzi iliichapa Real Sociedad ya Hispania mabao 2-0 karika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye uwanja wa Stamford Bridge.

Mshambuliaji mpya wa Chelsea, Diego Costa aliibuka nyota wa Chelsea baada ya kuifungia mabao yote mawili.

No comments:

Post a Comment