KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 13, 2014

ROONEY NAHODHA MPYA MAN UTD


KOCHA Mkuu wa Manchester United, Louis van Gaal, amemteua mshambuliaji nyota wa timu hiyo, Wayne Rooney kuwa nahodha mpya.

Van Gaal amemteua Rooney kushika wadhifa huo kutokana na kuvutiwa na kiwango chake cha soka tangu alipoanza kuinoa timu hiyo mwezi uliopita.

Kocha huyo raia wa Uholanzi amesema, siku zote kwake, chaguo muhimu ni nahodha wa timu na kwamba anaamini, Rooney atakuwa kiongozi mzuri wa wachezaji wenzake.

Wakati huo huo, Van Gaal ameendelea kuwapa raha mashabiki wa Manchester United, baada ya kuiongoza timu hiyo kuichapa Valencia ya Hispania mabao 2-1.

Mabao ya Manchester United yalipachikwa wavuni Darren Fletcher dakika ya 49 na Marouane Fellani aliyefunga bao l;a ushindi dakika ya 90.

Bao la Valencia lilipachikwa wavuni na Rodrigo, ikiwa ni dakika chache baada ya Rooney kukosa penalti baada ya shuti lake kuokolewa na kipa Diego Alves.

No comments:

Post a Comment