KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 28, 2011

FIVE STARS MPYA KUZALIWA KESHO

JOKHA Kassim

Mussa Kijoti

SAMIRA Rajabu




ZENA Mohamed


KIKUNDI cha taarab cha Five Stars kinatarajiwa kufanya onyesho la uzinduzi mpya, utakaofanyika kesho kwenye ukumbi wa hoteli ya Travertine, Magomeni, Dar es Salaam.
Kiongozi wa kikundi hicho, Ally J alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, maandalizi yote kwa ajili ya onyesho hilo yamekamilika.
Five Stars inafanya uzinduzi huo, kufuatia kuundwa upya baada ya wasanii wake 14 kufariki katika ajali ya gari, iliyotokea mapema mwaka huu Mikumi mkoani Morogoro.
Ally J alisema katika uzinduzi huo, wasanii wao wote wapya watapanda jukwaani, ikiwa ni pamoja na kuimba vibao vyao vipya, vitakavyokuwemo kwenye albamu yao ya kwanza.
Alivitaja vibao hivyo kuwa ni Mwenye hila habebeki, Watu na tabia zao, Ulaumiwe wewe nani, Silipizi ubaya, First Lady na Sina gubu nina sababu.
Miongoni mwa wasanii wapya wanaotarajiwa kupanda jukwaani leo ni pamoja na Mussa Kijoti na Mariam Mohamed, ambaye ni mshindi wa shindano la Bongo Star Search mwaka jana.
Waimbaji wengine wanaotarajiwa kupamba onyesho hilo ni pamoja na Jokha Kassim, ambaye alikuwepo kwenye kundi hilo kabla ya kujiengua.
Ally J amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia onyesho hilo kwa vile wamewaandalia vitu vya uhakika, ambavyo vitalifanya kundi hilo lirejee kwenye chati.

No comments:

Post a Comment