KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 4, 2016

YANGA YAZIDI KUNUSA UBINGWA


MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Yanga jana walijiweka kwenye nafasi nzuri ya kutetea taji lao baada ya kuibanjua Stand United mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Washambuliaji wa kimataifa, Donald Ngoma na Amis Tambwe ndio walioiwezesha Yanga kuibuka na ushindi huo mnono baada ya kuifungia mabao hayo matatu.

Ngoma alifunga bao la kwanza dakika ya pili kabla ya kuongeza la pili dakika ya 45. Tambwe alifunga bao la tatu dakika ya 63.

Stand ilifunga baola kujifariji dakika ya 81 lililofungwa na mshambuliaji Elias Maguli kwa mkwaju wa penalti baada ya Thabani Kamusoko wa Yanga kucheza rafu kwenye eneo la hatari.

Kutokana na ushindi huo, Yanga inaendelea kuongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 68, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 59 na Simba yenye pointi 58.


No comments:

Post a Comment