KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 4, 2016

UCHAGUZI MKUU YANGA SASA JUNI 25, FOMU KUANZA KUTOLEWA



KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imetangaza Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Yanga kuwa utafanyika Juni 25, 2016 badala ya Juni 5, 2016.
Kamati ya Uchaguzi ya TFF imelazimika kufanya hivyo kwa kuzingatia ushiriki wa Yanga ambayo inashiriki michuano ya kimataifa.
Sekretarieti ya Yanga ambayo ingefanya kazi kwa pamoja na Kamati ya Uchaguzi kwa kushirikiana na TFF kwa sasa inashughulikia pia kuiandaa timu kwa ajili ya michuano ya kimataifa.
Yanga inatarajiwa kucheza na Esperanca ya Angola katika michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika Mei 7, mwaka huu kabla ya kurudiana kati ya Mei 17 na 18, mwaka huu huko Angola.
Kwa mujibu wa ratiba mpya, fomu za kuwania uongozi wa Yanga zitaanza kuchukuliwa Mei 25, 2016 na kwamba uchaguzi huo utafanyika ndani ya muda ambao Serikali kwa kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) iliagiza uchaguzi kufanyika kabla ya Juni 26, 2016 hivyo uchaguzi utafanyika ndani ya wakati.
Katiba itakayotumika ni ya mwaka 2010 na kwamba Wanachama wa Yanga watatumia kadi za kawaida za uanachama na si za benki.


Wakati huo huo, Yanga itaanza kutoa fomu kwa ajili ya wanachama wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kuanzia Mei 27 badala ya leo kama ilivyotangazwa awali na Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit, amesema leo katika Mkutano na Waandishi wa Habari makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam, kwamba mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu hizo utakuwa ni Mei 29.
Kiongozi huyo alisema kuwa baada ya zoezi hilo Kamati ya Uchaguzi itaanza kusikiliza pingamizi zitakazokuwa zimewasilishwa huku orodha ya mwisho ya wagombea waliopitishwa ikitarajiwa kutangazwa Juni Mosi.
Aliongeza kuwa Juni Mosi hadi 4 itakuwa ni kipindi cha kampeni kwa wagombea waliopitishwa na uchaguzi mkuu utafanyika Juni 5 kwenye ukumbi utakaotangazwa hivi karibuni.
Alisema kuwa uchaguzi huo utasimamiwa na TFF baada ya kushindwa kufanya uchaguzi tangu mwaka 2014 muda wa viongozi waliokuwa madarakani ulipomalizika.
Kufanyika kwa uchaguzi huo kutatoa nafasi kwa viongozi wapya kusimamia usajili wa wachezaji kwa ajili ya msimu ujao wa ligi na kufanya mabadiliko mengine ya katiba kwa kufuata maelekezo ya TFF.

No comments:

Post a Comment